Player_logo Podcasts Community Create a Podcast
460>_632254

Cosmas Chidumule anafahamika kwa wengi kama Gwiji la Muziki wa Tanzania.Ni mtunzi na muimbaji wa vibao vingi vilivyopata umashahuri kwenye ulimwengu wa muziki.Baadhi ya vibao mashuhuri ni kama Neema, usitumie pesa kama fimbo, kifo na nalala kwa taabu. Pia ameimba na bendi nyingi mashuhuri kama butiama jazz, Vijana Jaz, Super Matimila, Dar International, Mlimani Park na wana Ndekule.Lakini hivi sasa Cosmas Chidumule ni mtu tofauti? Amebadilisha maisha yake kabisa. Je huyu Gwiji la Muziki ametokea wapi? Yuko wapi? Anaenda wapi? Kwa nini ameokoka? Nini kilitokea hadi kubadilisha maisha yake? Nini maoni yake juu ya muziki wa kizazi kipya Bongo Flava? Sikiliza zaidi.

[PLAY]